Home Masumbwi CARNELO aendeleza ubabe uzito wa kati.

CARNELO aendeleza ubabe uzito wa kati.

by Sports Leo
0 comments

Bondia wa Mexico Carnelo Alvarez amefanikiwa kutwaa ubingwa wa Unidisputed world super middleweight championships baada ya kumchapa kwa TKO bondia Caleb Plant usiku wa kuamkia leo.

Pambano hilo lilifanyika huko Las Vegas Marekani katika ukumbi maarufu wa MGM Arena lilishuhudia bondia huyo akimwangusha Mmarekani Caleb mara mbili katika raudi ya 11 na kumaliza mchezo.

                                                                           

banner

Canelo anakuwa bondia wa kwanza kwenye historia ya masumbwi kumiliki mikanda yote ya uzito wa kati.

Bondia huyo anayetokea katika kambi ya Floyd Maywether ameshinda jumla ya mapambano 57 akitoa sare mawili na kupigwa moja tu tangu aanze kupigana ngumi za kulipwa.

Mabondia wa zamani Mike Tyson na Manny Pacquiao wamemsifu na kumpongeza Canelo kwa kusema alikuwa mkali zaidi ya mpinzani wake na kwamba masumbwi yako salama mikononi mwake.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited