Connect with us

Masumbwi

CARNELO aendeleza ubabe uzito wa kati.

Bondia wa Mexico Carnelo Alvarez amefanikiwa kutwaa ubingwa wa Unidisputed world super middleweight championships baada ya kumchapa kwa TKO bondia Caleb Plant usiku wa kuamkia leo.

Pambano hilo lilifanyika huko Las Vegas Marekani katika ukumbi maarufu wa MGM Arena lilishuhudia bondia huyo akimwangusha Mmarekani Caleb mara mbili katika raudi ya 11 na kumaliza mchezo.

                                                                           

Canelo anakuwa bondia wa kwanza kwenye historia ya masumbwi kumiliki mikanda yote ya uzito wa kati.

Bondia huyo anayetokea katika kambi ya Floyd Maywether ameshinda jumla ya mapambano 57 akitoa sare mawili na kupigwa moja tu tangu aanze kupigana ngumi za kulipwa.

Mabondia wa zamani Mike Tyson na Manny Pacquiao wamemsifu na kumpongeza Canelo kwa kusema alikuwa mkali zaidi ya mpinzani wake na kwamba masumbwi yako salama mikononi mwake.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Masumbwi

  • Mwakinyo Huru

    Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini (TPBRC) imemfungulia bondia Hassan Mwakinyo kutoka kifungoni baada...

  • Bondia Mtanzania Fadhili Majiha ‘Kiepe Nyani’ ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC Afrika...

  • Ibrahim Class Amtwanga Mchina

    Bondia Mtanzania Ibrahim Class ameshinda pambano la ubingwa wa TPBRC dhidi ya bondia raia...

  • Mwakinyo Aitwa Mahakamani

    Kampuni ya PAF Promotion imemfungulia shauri la madai Bondia Hassan Mwakinyo ambalo linatarajiwa kutajwa...