Connect with us

Masumbwi

Kiduku amtaka aliyempiga Dulla Mbabe

Bondia Twaha Kiduku ameonesha nia ya kuhitaji pambano baina yake na bondia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Tshimanga Katompa ambaye alimpiga bondia mwingine wa Tanzania Abdallah Pazi maarufu kama Dulla mbabe siku ya Jumamosi katika pambano lililopewa jina la Kiboko ya Wageni.

Katika kuonesha kutofurahishwa kupigwa na kudhalilishwa kwa Dulla Mbabe,Twaha amewaomba mapromota wa ngumi nchini kuandaa pambano hilo mapema ili yeye aweze kurudisha heshima ya nchi.

Twaha Kiduku hajapigana tangu ampige Dulla mwezi Agosti mwaka huu na amesema kuwa atajiandaa vya kutosha kuhakikisha anashinda endapo pambano hilo likiwepo.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Masumbwi

  • Mwakinyo Huru

    Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini (TPBRC) imemfungulia bondia Hassan Mwakinyo kutoka kifungoni baada...

  • Bondia Mtanzania Fadhili Majiha ‘Kiepe Nyani’ ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC Afrika...

  • Ibrahim Class Amtwanga Mchina

    Bondia Mtanzania Ibrahim Class ameshinda pambano la ubingwa wa TPBRC dhidi ya bondia raia...

  • Mwakinyo Aitwa Mahakamani

    Kampuni ya PAF Promotion imemfungulia shauri la madai Bondia Hassan Mwakinyo ambalo linatarajiwa kutajwa...