Connect with us

Masumbwi

Bondia Mwingine Afariki Ulingoni

Bondia wa Marekani Patrick Day 27,ambaye alikuwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi tangu siku ya Jumamosi usiku baada ya kujeruhiwa vibaya katika pambano la ndondi ya kulipwa amefariki.

Bondia huyo alipigwa na mpinzani wake Charles Conwell akapoteza fahamu ulingoni katika roundi ya 10 katika pambano la Superwelter weight lililofanyika chicago nchini marekani ambapo alianguka na kupoteza fahamu mpaka alipofariki kutokana na majeraha katika ubongo ambapo alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya westernnorth memorial Hospital nchini humo lakini alifariki dunia.

Mwaka 2019 umekua mchungu kwa tasnia ya ngumi ambapo mpaka sasa mabondia watatu wamefariki ulingoni akiwemo day wengine bondia muajentina Hugo Santillan aliyefariki mwezi julai huku mburgalia Boris Stanchov akifariki mwezi wa tisa baada ya kupigwa ulingoni.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Masumbwi

  • Mwakinyo Huru

    Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini (TPBRC) imemfungulia bondia Hassan Mwakinyo kutoka kifungoni baada...

  • Bondia Mtanzania Fadhili Majiha ‘Kiepe Nyani’ ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC Afrika...

  • Ibrahim Class Amtwanga Mchina

    Bondia Mtanzania Ibrahim Class ameshinda pambano la ubingwa wa TPBRC dhidi ya bondia raia...

  • Mwakinyo Aitwa Mahakamani

    Kampuni ya PAF Promotion imemfungulia shauri la madai Bondia Hassan Mwakinyo ambalo linatarajiwa kutajwa...