Connect with us

Masumbwi

Mgunda Aondoka Simba sc

Kocha wa klabu ya Simba sc Juma Mgunda ameondoka klabuni hapo kwa ruhusa maalumu na kuamua kurejea nyumbani kwao jijini Tanga kutokana na matatizo binafsi ya kifamilia siku moja baada ya kocha mkuu wa klabu hiyo Roberto Oliveira “Robertinho” kurejea akitokea nyumbani kwao nchini Brazil.

Kuondoka kwa Mgunda kumepishana siku moja na kocha mkuu ambaye amerejea na kuchukua jukumu la kufanya maandalizi ya mwisho mwisho kuelekea mchezo dhidi ya Singida Big Stars siku ya kesho utakaofanyika jijini Dar es salaam ambapo Robertinho na msaidizi wake watashika timu bila Mgunda kwa mara ya kwanza tangu wachukue jukumu la kuinoa timu hiyo.

Simba sc itakabiliwa na upinzani mkali katika mchezo huo dhidi ya Singida Big Stars ambapo vikosi vya timu zote mbili vimefanya sajili za maana zikiwa na mastaa mbalimbali wenye makali ya kutosha kuonyesha burudani kwa wananchi na mashabiki mbalimbali.

Kila timu ina umuhimu wa kuchukua alama tatu katika mchezo huo baada ya awali kugawana alama katika mchezo wa duru ya kwanza katika uwanja wa Liti mjini Singida huku mpaka sasa Simba sc ina alama 50 nafasi ya pili na Singida Big Stars ikiwa na alama 43 nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu nchini.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Masumbwi

  • Mwakinyo Huru

    Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini (TPBRC) imemfungulia bondia Hassan Mwakinyo kutoka kifungoni baada...

  • Bondia Mtanzania Fadhili Majiha ‘Kiepe Nyani’ ambaye ni bingwa wa mkanda wa WBC Afrika...

  • Ibrahim Class Amtwanga Mchina

    Bondia Mtanzania Ibrahim Class ameshinda pambano la ubingwa wa TPBRC dhidi ya bondia raia...

  • Mwakinyo Aitwa Mahakamani

    Kampuni ya PAF Promotion imemfungulia shauri la madai Bondia Hassan Mwakinyo ambalo linatarajiwa kutajwa...