Connect with us

Soka

Newcastle Utd kung’oa wanne Man Utd

Baada ya kununuliwa na familia ya kifalme ya Saudi Arabia chini ya mwana mfalme Bin Sueiman klabu ya soka ya Newcastle United ya Uingereza imeanza mipango kabambe ya usajili kuanza kuisuka timu hiyo kuwa ya ushindani zaidi kwenye ligi kuu ya soka nchini Uingereza.

Klabu hiyo imwewaka kwenye rada zao wachezaji wanne wa Manchester United beki Eric Baily aliepoteza namba baada ya ujio wa Rafael Varane kutoka Real Madrid,viungo Jesse Lingard na Don Van De Beek ambao wamekosa dakika za kutosha uwanjani pamoja na mshambuliaji Anthony Martial anayesugua benchi kwasasa.

Timu hiyo pia ipo kwenye mipango ya kumuajiri Ralph Rangnick kuwa Mkurugenzi mpya wa michezo wa klabu hiyo kusuka idara ya usajili lutokana na uzoefu wake kufanya kazi RB Leipzig ya Ujerumani.

Mabosi wa timu hiyo wapo kwenye mipango ya kumtimua kocha mkuu wa timu hiyo Steve Bruce huku makocha Antonio Conte,Steven Gerrard na brendan Rodgers wakiwa kwenye mipango yao.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka