Connect with us

Makala

Israel Aongeza Mkataba Simba Sc

Ikiwa katika maboresho makubwa ya kikosi chake,Klabu ya Simba Sc imefanikiwa kumuongeza mkataba beki Israel Mwenda mpaka mwaka 2026 ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili kusalia klabuni hapo.

Simba Sc imeona umuhimu wa kumbakisha beki huyo ambaye mkataba wake wa miaka miwili ulikua unafika tamati Juni 30 mwaka huu ambapo katika dili hilo jipya staa huyo amefanyiwa maboresho katika fedha ya kusaini mkataba (Signing on fees) na mshahara pamoja na bonansi mbalimbali.

Beki amebakishwa kutokana na umuhimu wake kikosini ambapo anaweza kucheza nafasi za beki wa pembeni zote mbili huku akiwa na uwezo wa kutumika kama kiungo wa ulinzi ama winga wa kulia ambapo amekua na kiwango kizuri pamoja na kutopata muda wa kutosha wa kucheza.

Israel alijiunga na Simba sc msimu wa 2021 ambapo mpaka sasa ameitumikia klabu hiyo kwa misimu mitatu akiwa mbadala wa Shomari Kapombe katika eneo la beki wa kulia.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala