Connect with us

Makala

Kuhusu Ugali Humwambii Kitu-Morrison

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga,Bernard Morrison amesema kuwa miongoni mwa vyakula ambavyo anapenda kula ni ugali.

Mghana huyo alitua Desemba akitokea nchini Ghana kwenye usajili wa dirisha dogo ambapo baada ya kutua amefanikiwa kuzitungua timu kama Tanzania Prisons,kwenye mchezo wa kombe la shirikisho huku Lipuli,Mbeya City na Simba alizitungua kwenye mechi za ligi kuu Bara.

Morrison mpaka sasa amecheza jumla ya mechi 10 amefunga mabao matatu ndani ya ligi kuu bara huku akiwa na bao moja kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho.

“Kwa sasa ninaendelea na mazoezi binafsi ili kulinda kipaji changu ili ligi ikirejea niwe kwenye kiwango ubora,ila katika chakula ninachopenda kula wakati huu nikiwa nyumbani ni Ugali kwani ninaufurahia ninapokula na unanipa nguvu pia unanifanya najisikia vizuri

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala