Connect with us

Makala

Kali Ongara Atua Kmc

Klabu ya Kmc imekamilisha usajili wa Kocha wa zamani wa klabu ya Azam Fc Kally Ongara akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Kocha Abdulhamid Moalin ambaye amejiuru siku chache zilizopita.

Kally ametambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari mapema hii leo ambapo atakua na jukumu la kuhakikisha anairudishia Kmc makali yake katika ligi kuu ya Nbc nchini.

Kally ambaye amewahi kuifundisha Azam Fc kwa nyakati tofauti tofauti amesaini mkataba huo mbele ya Meya wa Halmashauri ya Kinondoni ndugu Songoro Mnyonge na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi Hanifa Selemani.

Mkataba huo haujawekwa wazi utakua wa muda gani na huku taarifa zikisema kuwa Kmc imeamua kumuajiri kocha huyo kutokana na kuridhika na falsafa zake ambapo mabosi hao pamoja na kuwa na rundo la Cv waliamua kumchagua kocha huyo.

Katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini mpaka sasa Kmc imevuna alama 14 ikicheza michezo 11 ya ligi kuu huku ikiwa na wastani wa -3 wa mabao ya kushinda na kufungwa.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala