Connect with us

Makala

Singida Big Stars Vs Yanga sc Kupigwa Zanzibar

Klabu ya Singida Black Stars imeamua kuupeleka mchezo wake wa ligi kuu dhidi ya Yanga sc katika uwanja wa Amaani Visiwani Zanzibar ili kupisha ukarabati unaoendelea katika uwanja wake wa nyumbani wa Ccm Liti.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika Visiwani humo siku ya Oktoba 30 mwaka huu ambapo kwa mujibu wa Kanuni za ligi kuu nchini,Klabu zinaruhusiwa kucheza michezo miwili ya nyumbani nje y viwanja vyao vya nyumbani ambapo wanapaswa kutoa taarifa ya maandishi mapema kabisa.

Mchezo huo unatarajiwa kuwa na mvuto kutokana na ubora mkubwa Black Stars ambao msimu huu wameboresha kwa kiasi kikubwa kikosi chao chini ya kocha Patrick Aussems.

Singida Black Stars mpaka sasa imefikisha alama 16 kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini baada ya kucheza michezo sita huku Yanga sc ikiwa katika nafasi ya nne alama 12 baada ya kucheza michezo minne ya ligi kuu ya Nbc nchini.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala