Connect with us

Makala

Medo Mbioni Kutua Kagera Sugar

Uongozi wa Klabu ya Kagera Sugar Umefungua mazungumzo na Kocha wa sasa wa klabu ya Mtibwa Sugar raia wa Marekani Mellis Medo ili kujiunga na klabu hiyo kuchukua nafasi ya kocha Paul Nkata.

Kwasasa kikosi cha Kagera Sugar kipo chini ya kaimu Kocha Bube na hii ni baada ya kufutwa kazi kwa Aliyekuwa Kocha wao Mkuu Paul Nkata na benchi lake lote la Ufundi.

Mazungumzo baina ya Uongozi wa Kocha Mellis Medo na Uongozi wa klabu ya Kagera Sugar Yanaendelea vizuri ambapo siku ya jana kocha Medo aliwaaga wachezaji wa klabu ya Mtibwa Sugar.

Medo anatarajiwa kusafiri kuelekea Kagera siku ya leo ili kumalizana na mabosi wa klabu hiyo na kutangazwa rasmi kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo ambapo atakuja pamoja na benchi lake la ufundi.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala