Connect with us

Makala

Feisal Aweka Ngumu Yanga sc

Pamoja na kwamba amewasilisha barua ya kutaka kuondoka klabuni hapo ikiwemo kulipa kiasi cha shilingi milioni 112 kama fidia ya kuvunja mkataba bafdo staa huyo amegoma kufanya mazungumzo ya aina yeyote na mabosi wa klabu hiyo ambao wamekua wakihaha kumtaka abadilishe mawazo.

Feisal tayari inasemekana ameshamwaga wino wa kuitumikia Azam Fc huku akipewa mshahara wa kiasi cha shilingi milioni 17 kwa mwezi ambao ni mara nne ya shilingi milioni nne anazolipwa sasa Yanga sc na tayari mpaka sasa hajalipoti kambini baada ya kutoweka siku chache zilizopita.

Feisal alisaini mkataba wa miaka minne ambao unapaswa kumalizika juni 30,2024 lakini ametumia mwanya huo kuvunja mkataba japo kumekua na sintofahamu endapo Yanga sc wakiamua kuchukua hatua zaidi za kisheria ambapo mpaka sasa inasemekana mabosi wa klabu hiyo tayari wamezirudisha fedha hizo pamoja na kumuandikia barua staa huyo aheshimu mkataba huku mamlaka kama Shirikisho la soka nchini pia likijulishwa.

Viongozi kadhaa wa serikali ambao ni mashabiki wa klabu ya Yanga sc akiwemo Waziri wa fedha Mh.Mwigulu Nchemba na Ridhiwani Kikwete wamejaribu kumshawishi staa huyo lakini wameshindwa baada ya kuendelea kusimamia msimamo wake huo na mpaka sasa hajaripoti kambini.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala