Connect with us

Soka

Muuaji Wa Simba Ajiuzuru Yanga

Mkurugenzi wa ufundi wa klabu ya Yanga sc Nassoro Jaylan amejiuru wadhifa huo ili kuwa karibu zaidi na familia yake iliyoko nchini Uingereza.

Jaylan mwenye asili ya Zanzibar makazi yake yapo nchini Uingereza na alikua kifanya kazi na Yanga kwa chinichini kutokana na kutokua na kibali cha kazi ambacho klabu hiyo ilikua inashughulikia mpaka alipoamua kujiudhuru.

Mtaalamu huyo ndio aliyesuka mipango ya kuifunga klabu ya Simba sc katika mchezo wa machi 8 huku pia akifanikiwa kutoa sare katika mchezo wa awali na alikua akishiriki kumpa mbinu mwalimu Luc Eymael.

Kwa mujibu wa klabu ya Yanga sc ni kweli wamepokea barua hiyo japo wamegoma kulitolea ufafanuzi zaidi mpaka uongozi utakapokaa.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka