Connect with us

Soka

Dirisha Dogo Hakukaliki Yanga

Mabosi wa Yanga wanafanya kila liwezekanalo kumalizana mapema na mabosi wa Tanzania Prisons ili kuwasajili nyota wawili wa timu hiyo winga Ismail Aziz na kiungo Cleophas Mkandala

Dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa Jumatatu ijayo, pengine mchakato wa kuwanasa nyota hao utakamilishwa wiki hiyo

Nyota hao ni miongoni mwa wachezaji waliopendekezwa na kamati ya Ufundi miongoni mwa wachezaji wa ndani

Aidha Yanga pia inamuwania beki wa Coastal Union Bakari Mwamnyeto ikimuhitaji beki huyo kwa mpango wa muda mrefu

Kwa upande wa safu ya ushambuliaji, Daruweshi Saliboko na Tariq Seif Kiakala ni miongoni mwa nyota wanaotajwa huku nyota wengine wa kigeni wakiendelea kufanya majaribio

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka