Connect with us

Makala

Uwanja Wa Azam Complex Wakamilika

Uongozi wa Azam Fc umesema kuwa tayari ukarabati wa Uwanja wa Azam Complex umekamilika kwa asilimia zote ukiwa sawa na ule wa TP Mazembe.

Ofisa Habari wa Azam FC, Zaka Zakazi amesema kuwa ubora wa uwanja huo kwa sasa ni wa kimataifa tofauti na ule wa mwanzo,hivyo baada ya ligi kuu kurudi baada ya kusimamishwa ana matumaini makubwa wachezaji wake watafurahia kufanya mazoezi kwenye uwanja huo.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona na wakati ukifanyiwa marekebisho Azam FC walikuwa wanatumia Uwanja wa Uhuru na Taifa kwa mechi zao za nyumbani.

““Uwanja wetu ubora wake upo sawa na ule uwanja wa TP Mazembe ya Congo kwa sasa upo hatua ya kimataifa hivyo tunajivunia kukamilisha ukarabati wetu kwa sasa”alisema Zaka Zakazi.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala