Connect with us

Soka

Song Akalia Kuti Kavu Cameroon

Baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Nigeria katika michuano ya mataifa ya Afrika (Afcon 2024) katika hatua ya 16 bora kocha wa timu ya Taifa ya Cameroon Rigobert Song amekalia kuti kavu kuendelea kuifundisha timu hiyo.

Mashabiki wengi nchini humo wameonyesha kutoridhishwa na kiwango cha timu hiyo na hivyo kusababisha kulalamika wakimlaumu Eto’o ambaye na Rais wa Shirikisho la soka nchini humo kuwa anatumia urafiki wake na Song na kushindwa kumtimua hata kama timu hiyo imefanya vibaya.

Song anaweza kuwa na wakati mgumu zaidi kuliko makocha wote waliobaki na kuna hofu kuwa anaweza kuondolewa kwenye nafasi hiyo baada pia kushindwa kufanya vizuri kwenye Kombe la Dunia 2022.

Kocha huyo ambaye alitwaa ubingwa wa Afcon mara mbili akiwa mchezaji wa Cameroon, amesema bado hajafanya uamuzi wa nini cha kufanya baada ya kutolewa Afcon.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka