Connect with us

Soka

Stars Yawarejesha Saba Simba sc

Mastaa saba waliokua na timu ya Simba sc nchini Afrika Kusini wanatarajiwa kurejea nchini kesho ili kujiunga na kambi ya timu ya taifa (Taifa stars) inayojiandaa na mchezo wa kufuzu michuano ya Afrika kwa wachezaji wa ndani(Chan) dhidi ya Kenya.

Mastaa hao walioitwa kikosini na kaimu kocha mkuu Ettiene Ndayiragije akisaidiana na Seleman Matola ni Jonas Mkude,Ibrahim Ajib,Gadiel Michael,Hassan Dilunga,John Boko,Aishi Manula na Erasto Nyoni.

Kwa mujibu wa Afisa Mtendaji mkuu wa klabu hiyo wachezaji hao wameshindwa kusafiri leo kutokana na kukosekana kwa ndege ya Atcl ambayo kwa mujibu wa ratiba zake itasafiri kesho kuja nchini.

Simba sc imeweka kambi nchini Afrika Kusini kujiandaa na michuano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa na kurejea kwa wachezaji hao bila shaka kutaathiri programu ya mwalimu Patrick Asseums ambaye timu yake itavaana na Ud Songo ya Msumbiji katika hatua ya awali ya michuano ya kimataifa.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka