Connect with us

Soka

Saido Amfurahisha Kaze

Kocha mkuu wa Yanga, Cedric Kaze amefurahishwa na kiwango cha mchezaji wake mpya Saido Ntibazonkiza alichokionyesha katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida United.

Kaze aliyemsajili mchezaji huyo ukiwa na usajili wake wa kwanza amesema kiwango alichokionyesha mchezaji wake anakifurahia kwani ameongeza kitu katika timu yake.

“Saido ni mchezaji mzuri na ameongeza kitu kwenye kikosi, ni mchezaji kiongozi na ameongoza vyema wachezaji wenzake”.

Saido alicheza mchezo wake wa kwanza katika mchezo huo na kufanikiwa kufunga mabao mawili huku akitoa pasi za kufunga zaidi ya tano lakini umakini mdogo wa Waziri Junior na Ditram Nchimbi ulisababisha kukosa mabao ya wazi.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka