Connect with us

Soka

Lukaku aomba radhi

Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Ubelgiji na Chelsea Romelu Lukaku hatimaye amemaliza tofauti zake na kocha mkuu wa timu hiyo Thomas Tuchel kwa kuomba msamaha na kurudishwa kikosini.

Mchezaji huyo aliondolewa kwenye kikosi kilichocheza na Liverpool kutokana na kuvuja kwa mahojiano yake na kituo cha skysports iliwekwa wazi kuwa mchezaji huyo hana furaha na hafurahishwa na jinsi kocha wake anavyomtumia katika kikosi hicho cha mabingwa wa kombe la klabu bingwa Ulaya.

Kocha Tuchel alisema kuwa aliamua kumuweka nje Lukaku ili kutokuchafua hali ya hewa ndani ya timu hiyo na kuwa makelele yaliyotokea kutoka kwenye vyombo vya habari hayakuwa na afya ndani ya kikosi chao.

Baada ya hapo mshambuliaji huyo alianza kuhusishwa na kuondoka ndani ya timu hiyo kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.

Lakini baada ya kikao cha mwalimu na mchezaji pamoja na maamuzi ya bodi wameamua kuwa mchezaji huyo ataendela kusalia na wala hawana mpango wa kumuuza.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka