Connect with us

Soka

Kuna Mourinho,Kuna Kocha

Jose Mourinho ameithibitisha dunia kuwa yeye ni zaidi ya kocha baada ya kufanikiwa kuiongoza Tottenham kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Westham united ukiwa na mchezo wa kwanza kwa kocha huyo tangu atangazwe kocha mpya wa timu hiyo akichukua nafasi ya Mouricio Pochetino.

Son alikua wa kwanza kuipatia bao Tottenham dakika ya 39 huku bao la pili likipachikwa na Lucas Moura dakika ya 43 na kufanya timu hiyo kwenda mapumziko ikiwa inaongoza.

Kipindi cha pili Harry Kane alifanikiwa kufikisha mabao saba baada ya kufunga bao la tatu dakika ya 49 na kuhakikisha pointi tatu kwa Mourinho baada ya Spurs kuwa na ushindi wa kusuasua siku za karibuni.

West Ham ilizinduka dakika ya 73 na kupachika bao lao la kwanza kupitia kwa Michail Antonio kabla ya lile la pili kupachikwa dakika ya 90+6 na Angelo Ogbonna.

Ushindi huo unaifanya Tottenham Hotspur kuwa nafasi ya 9 ikishinda mchezo wake wa nne na inafikisha jumla ya pointi 17 kwenye msimamo wa Ligi Kuu England

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka