Connect with us

Soka

Kocha Mbabe Wa Zahera Atimuliwa

Klabu ya Wydad Casablanca ya Morocco imemfuta kazi kocha wake Mkuu Sebastian Desabre mwezi mmoja tu tangu imteue kushika nafasi hiyo.

Tukio hilo limekuja baada ya Wydad kupoteza mchezo wake wa ligi wikiendi hii  na klabu ya Difaa El-Jadid kwa Bao pekee la Winga Simon Msuva na baada ya mechi hiyo Desabre amefukuzwa baada ya kuwa na matokeo yasiyoridhisha.

Desabre ndiye aliyeiongoza Pyramids Fc kuwafunga Yanga iliyokua chini ya Mwnyi Zahera nyumbani na ugenini katika michuano ya kombe la shirikisho na kuhitimisha safari ya kocha Mwinyi Zahera katika michuano ya kimataifa akiwa Yanga.

Kocha huyo ni kama amekuwa na mkosi kwa sasa kwani anafukuzwa mara ya pili ndani ya msimu huu, hii ni baada ya kufukuzwa na Pyrmids Fc ambayo licha ya kufanya vzuri katika kombe ka shrikisho barani Afrika, kiu yao kubwa ilikuwa pia katika ligi ya nchini Misri.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka