Connect with us

Soka

Juuko Aweka Ngumu Simba

Beki wa klabu ya Simba Mganda Juuko Murshid ameweka ngumu kuripoti klabuni kujiunga na timu katika kambi ya maandalizi ya msimu akishinikiza kuachwa ajiunge na timu nyingine.

Mchezaji huyo aliyeiongoza Uganda katika michuano ya mataifa ya Afrika(Afcon 2019) yanayofanyika nchini Misri imedaiwa kuwa hana mpango wa kuendelea na klabu hiyo hivyo anashinikizwa kuachwa ili atafute timu nyingine ingali bado ana mkataba na mabingwa hao mara mbili mfululizo wa ligi kuu ya Tanzania bara.

Akizungumza na Wanahabari Afisa mtendaji mkuu wa klabu hiyo Crescentius Magori alithibitisha kukata mishahara ya mchezaji huyo kama adhabu ya utoro aliyoionyesha klabuni hapo.

Juuko  26 alisajiliwa na Simba misimu kadhaa iliyopita licha ya kujihakikishia namba katika kikosi cha timu ya taifa ya Uganda(The cranes) amekua na wakati wa kusuasua katika klabu ya simba kutokana na matatizo ya kinidhamu likiwemo suala la utoro.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka