Connect with us

Soka

Je United Imeuzwa?

Mwandishi wa habari wa saudi Arabia Moaid Mahjoub ni mtu pekee ambae ndo aliyevujisha habari kuwa klabu ya manchester United imeuzwa kwa matajiri wa kiarabu wakiongozwa na mtoto wa mafalme wa nchi hiyo Mohammed Bin Salman.

Inataarifiwa kuwa Wawakilishi wakuu wa United wameonekana huko nchini Saudia juzi Alhamis mna habari zinazosambaa kwa sasa ni kuwa wawakilishi hao walienda Saudi kwajili ya kukamilisha uuzwaji wa klabu hiyo kutoka kwa Wamarekani familia ya Glazzers ambao wanaimiliki klabu hiyo toka mwaka 2005.

Bado watu wengi wanaendelea kuhoji kuhusu taarifa hizo kutoka Saudi Arabia husasani aliyetoa taarifa hizo ambaye ni mfanyakazi kutoka mamlaka za mambo ya nje nchini humo. mashabiki wa Manchester United huku wengi wakisubiria taarifa rasmi kutoka katika klabu ya manchester utd au wawakilishi wa united waliopo huko japo wengi wanaomba taarifa hizo ziwe kweli ili usajili bab’kubwa ufanyike kuboresha kikosi hicho.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka