Connect with us

Soka

Billo akiwesha Alliance

Aliyekua kocha mkuu wa klabu ya Alliance ya jijini Mwanza Athuman Bilal “Billo”ameamua kuachana na klabu hiyo baada ya kuiongoza katika mechi moja ya ligi kuu pekee.

Kocha huyo aliyejiunga na timu hiyo akitokea Stand united ya mjini Shinyanga ameachana na klabu hiyo kwa madai ya kukataa kuingiliwa majukumu yake.

“Nilitaka kuondoka kabla ya mechi na Mbao fc lakini nikatumia busara zangu Kubaki na kukiongoza kikosi cha Alliance kwa mechi hiyo tu moja, kwani nilitaka kulinda heshima yangu kwa kuachana na klabu hiyo ambayo ni ngumu mno kuifundisha.”alisema Billo

Billo ni miongoni mwa makocha maarufu jijini Mwanza na kanda ya ziwa kwa ujumla kutokana na kufanikiwa kuzifanya timu anazozifundisha kuwa ngumu kufungika hasa zinapocheza na timu kubwa kama Simba na Yanga.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka