Connect with us

Soka

Anderson Atundika Daruga

Staa wa zamani wa Manchester united Anderson Oliveira amestaafu kucheza soka la ushindani akiwa katika klabu ya Adama Demirspor inayoshiriki ligi daraja la pili nchini uturuki.

Staa huyo mshindi wa kiatu cha dhahabu mwaka 2007 alihamia manchester united akitokea Fc Porto ya Ureno ambako alionyesha uwezo mkubwa akitokea Gremio ya kwao nchini Brazil.

Licha ya kuaminiwa mara kadhaa na kocha Alex Ferguson Anderson alishindwa kuwa na ubora unaofanana kwa muda mrefu huku majeruhi yakichangia hali iliyosababisha kuachana na united mwaka 2015 na kujiunga na As Roma ambako hakudumu na kurudi nchini kwao katika klabu ya Internacional.

Licha ya kuitumikia timu hiyo katika michezo 11 msimu uliopita staa huyo atabakia klabuni hapo akipewa kazi katika klabu hiyo baada ya kukubali kupunguziwa mshahara wake na ataangwa rasmi tarehe 12 october.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka