Connect with us

Makala

Job Arejeshwa Taifa Stars

Kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania Hemed Morocco amemrejesha kikosini beki wa klabu ya Yanga sc Dickson Job baada ya kumtema kutokana na tatizo la utovu ws nidhamu wakati wa michuano ya Afcon 2023 nchini Ivory coast.

Morocco ametaja kikosi cha mastaa 23 kujiandaa na michezo miwili ya kuwania kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka 2025 dhidi ya Guinea na Ethiopia.

Job amerejeshwa baada ya kuomba msamaha kutokana na kosa la kukataa kuchezeshwa kama beki wa kulia katika michuano ya Afcon iliyofanyika nchini Ivory coast na Stars kutolewa katika hatua ya makundi.

Kocha Hemed Morocco ameendelea na msimamo wake wa kumtumia mchezaji huyo kama beki wa kulia ama beki wa pembeni katika mfumo wa mabeki watatu wa kati.

Mbali na Dickson Job pia mastaa wengine sita kutoka Yanga sc wameitwa kujiunga na Taifa Stars wakiwemo AbouTwalib Mshery,Nickson Kibabage,Bakari Mwamnyeto,Mudathir Yahaya,Ibrahim Hamad na Clement Mzize.

Mastaa kutoka klabu za Simba sc,Azam Fc na Yanga sc wamejumuika na mastaa wanaocheza nje ya nchi pamoja na baadhi ya timu za ligi kuu kuunda kikosi cha mastaa 23 watakaoingia kambini kwa ajili ya michezo hiyo itakayofanyika mwanzoni mwa Septemba mwaka huu.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala