Connect with us

Makala

Coastal Wajihakikishia Ushindi Kwa Yanga

Coastal Union ambao watamenyana leo Octoba,3 na Yanga Sc uwanja wa Mkapa jijini Dar-es-salaam wamejihakikishia kuchukua pointi tatu muhimu leo katika mchuano huo utakaochezwa majira ya saa 1:00 usiku.

Kocha Mkuu wa Coastal Union, Juma Mgunda amesema  kuwa maandalizi ya kikosi yapo vizuri na wanaamini watapata pointi tatu kwenye mchezo huo kwani lengo ni kushinda na kunyakua alama tatu muhimu.

Coastal Union inakutana na Yanga ikiwa imepoteza mechi mbili ndani ya ligi na kupata sare moja na kushinda mchezo mmoja huku Yanga ikiwa imeshinda mechi tatu na kupata sare moja mbele ya Tanzania Prisons kwa kufungana bao 1-1 Uwanja wa Mkapa.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala