Connect with us

Makala

Beki Simba Azipa Kipaumbele Azam,Yanga

Aliyekuwa beki wa Simba  Sc Zana Coulibaly ambaye pia ni raia wa Ivory Coast amesema kuwa yupo tayari kurejea Bongo kukipiga ndani ya Yanga auAzam iwapo watahitaji huduma yake.

Beki huyo alidumu Simba kwa miezi tisa kabla ya kuondoka na kujiunga na AS Vita ya DR Congo kwa mkataba wa miaka miwili katika michuano ya kimataifa amefanikiwa kucheza mechi tatu pekee msimu huu.

Coulibaly amesema kuwa moja kati ya sehemu ambazo hawezi kuzisahau kirahisi ni Tanzania na yupo tayari kurejea kwa kujiunga na timu yoyote zikiwemo Azam na Yanga kutokana na ukarimu wa watu wake.

“Natamani kuona narudi tena huko kucheza haijalishi ni timu gani iwe kama Azam au hata Yanga wakinihitaji nitakuwa tayari kurejea,” amesema Coulibaly.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala