Connect with us

Makala

Arsenal Aitungua Liverpool Mabao 2-1

Juhudi za wachezaji wa Arsenal uwanjani siku ya jana umewasaidia  mbele ya mabingwa wa ligi kuu England,Liverpool baada ya kuwafunga mabao 2-0 katika uwanja wa nyumbani Emirates.

Mabao ya Arsenal yalipachikwa na Alexandre Lacazette dakika ya 32 na Reiss Nelson dakika ya 44 huku bao lililofungua mchezo kwa upande wa Liverpool lilifungwa na Sadio Mane dakika ya 20.

Kocha mkuu Arsenal,Mikel Arteta amesema kuwa haikuwa kazi rahisi kupata ushindi mbele ya mabingwa kwani wana timu imara ya ushindani ambayo imewapa ubingwa ila vijana wake walikuwa na juhudi mchezoni jambo lililowapa matokeo mazuri.

“Kucheza na mabingwa na kupata matokeo ni jambo jema hii inatupa picha ya kujua kule ambako tunakwenda kama si kwa wakati huu basi itakuwa kwa ajili ya wakati ujao” alisema Arteta

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala