Connect with us

Makala

Abdul Afungukia Kiwango Chake

KAMWE hauwezi kuwataja mabeki bora wa pembeni, namba mbili bila ya kulitaja jina la Juma Abdul anayeichezea Yanga ambaye alijiunga nayo msimu wa 2011/ 2012 akitokea Mtibwa Sugar ya Manungu, Morogoro.

Wakati Abdul anajiunga na Yanga alikutana na upinzani mkubwa kutoka kwa aliyekuwa nahodha wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa na baadaye Godfrey Taita aliokuwa anacheza nao nafasi moja.

Awali, Abdul wakati anajiunga na Yanga hakuwa anapata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza, lakini baadaye akawa anapata baada ya kuaminika na waliokuwa makocha wa timu hiyo Mholanzi, Ernie Brandts, Sam Timbe, Tom Saintifiet na Hans Pluijm.

Baada ya kuaminika na kupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza, beki huyo akapewa unahodha kama nahodha msaidizi msimu wa 2017/ 2018, cheo ambacho anaendelea nacho hivi sasa.

Beki huyo kwenye msimu huu ameonekana kurejea kwa kasi kubwa akicheza michezo mitatu mfululizo ya Ligi Kuu Bara tangu arejee ambayo yote imepata ushindi walipocheza na Coastal Union, Mbao FC na wikiendi iliyopita wakawafunga Ndanda FC.

Abdul amerejea uwanjani kwenye msimu huu akitokea kwenye majeraha ya enka yaliyomuweka nje ya uwanja msimu mzima uliopita kabla ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mkongomani, Mwinyi Zahera kumuamini Paul Godfrey ‘Boxer’ kwa kumpa nafasi ya kucheza na kuwa tegemeo katika timu ambaye hivi sasa yupo akiuguza majeraha ya goti.

Habari kwa msaada wa Yanga whatsapp makao makuu

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala