Connect with us

Soka

Mkuchika Aipeleka Yanga Bungeni

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora Kapteni George Mkuchika ameifagilia klabu ya Yanga sc bungeni baada ya kuifunga Simba sc katika mchezo wa watani wa jadi uliofanyika mapema mwaka huu.

Waziri huyo ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya wadhamini ya klabu hiyo aliichomekea klabu yake hiyo wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Licha ya kuitaja mara nne katika hotuba hiyo pia aliipongeza klabu ya Yanga kwa kufanya vizuri katika michezo miwili ya watani wa jadi licha ya kuelekea kuukosa ubingwa kutokana na kuachwa pointi nyingi na watani wao Simba.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka