Connect with us

Soka

Ziyech Mikononi Mwa Lampard

Kocha wa klabu ya Ajax Amsterdam, Eric Tel Hag, amethibitisha kuwa kiungo wake, Hakim Ziyech, atajiunga na klabu ya Chelsea mwishoni mwa msimu baada ya pande mbili kufikia makubaliano.

Ajax na Chelsea wamefikia makubaliano ya ada ya kiasi cha paundi milioni 38, ili kufanikisha dili hilo la kiungo huyo mshambuliaji raia wa morocco

Ziyech ambaye ni kiungo mshambuliaji asilia akiwa na uwezo wa kucheza kulia na kushoto aliisaidia Ajax kutinga hatua ya nusu fainali ya Uefa Champions League msimu uliopita huku akicheza mechi 49 na kufunga mabao 21 na kuasisti mabao 24 katika michuano yote.

Licha ya kusaidia Ajax kutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Uholanzi pia ameifungia timu hiyo mabao 48 na kusaidia upatikanaji wa mabao 82 katika mechi 160 alizoichezea timu hiyo.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka