Connect with us

Soka

Man Utd Yakomaa na Sancho

Klabu ya Manchester united inaamini itaipiku Chelsea kwenye mbio za kuwania saini ya Kiungo mshambuliaji na winga Jodan Sancho anayechezea klabu ya Dortmund ya Ujerumani.

Jordan Sancho anadaiwa kuwa na thamani ya Pauni milion 120 ambapo klabu yake ya Dortmund ipo tayari kumuuza kwa timu itakayofikia thamani hiyo kwa mchezaji waliyemnunua kwa Paundi milioni 8 kutoka Manchester city.

United haina budi kukabiliana na Chelsea katika mbio za kumuwania winga huyo ambaye inaonekana angependelea zaidi kurudi nyumbani huku kocha Frank Lampard akiwa na ubavu wa kushindina na United baada ya kuwa hela za kutosha baada ya kutosajili kwa madirisha mawili yaliyopita.

Manchester United wanapewa kipaumbele kumsajili mchezaji huyo aliyeweka rekodi ya kufunga mabao 25 kabla ya kufikisha umri miaka 20 katika ligi ya bundesliga baada ya kumuandalia malipo mazuri huku Mtendaji mkuu wa klabu hiyo Ed Woordward akiahidi uwekezaji wa kutosha katika kikosi hicho.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka