Connect with us

Soka

Kanda Awatisha Yanga

Staa wa klabu ya Simba sc Deo Kanda amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga sc utakaofanyika jioni ya leo katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Kanda amesema kuwa licha ya Yanga kuwa na mabeki imara wakiongozwa na Kelvin Yondan hilo haliwatishi na kushindwa kuibuka na ushindi katika mchezo huo wa ligi kuu.

“Tunakwenda kucheza na Yanga ni wazuri  wameimarika hasa eneo la ulinzi ila hilo haltufanyi tushindwe kufanya vizuri.Tunajua ngome hiyo inamtegemea Yondani na wenzake lakini kama washambuliaji tupo vizuri mno na hawataamini tutakachowafanyia taifa kwenye dabi.

Kanda amesajiliwa na Simba kwa mkopo akitokea Tp Mazembe ya kongo na siku za karibuni amekua na kiwano bora akifunga mabao mawili katika mechi mbili mfululizo.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Soka