Friday, May 9, 2025
Home Makala Prisons,Singida Big Stars Wafungiwa

Prisons,Singida Big Stars Wafungiwa

by Sports Leo
0 comments

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetoa adhabu ya kutosajili kwa kipindi cha dirisha moja kwa klabu za Singida Big Stars na Tanzania Prisons Fc baada ya vilabu hivyo kusajili Wachezaji wenye mikataba na klabu nyingine bila kufuata taratibu husika za usajili.

Klabu ya Singida Big  Stars iliyopanda daraja la ligi kuu msimu huu ilimsajili golikipa Metacha Mnata akitokea klabu ya Polisi Tanzania bila kufuata taratibu huku akiwa na mkataba ambao ulikua bado haujaisha na huku klabu ya Prisons Fc yenyewe ilimsajili golikipa Musa Mbise wa Coastal Union ambaye nae alikua na mkataba na klabu hiyo bila kufuata taratibu za kawaida za usajili.

Kutokana na adhabu hizo klabu hizo zitakosa kushiriki katika dirisha dogo la usajili linalotarajiwa kufunguliwa mwezi desemba mwaka huu ambapo klabu nyingine zitatumia muda huo kufanya maboresho ya vikosi vyao kutokana na usajili waliofanya katika dirisha kubwa la usajili.

banner

Kamati imezikumbusha Klabu zote Nchini kuwa usajili wa Wachezaji unafanywa kwa kuzingatia Kanuni, na ambazo zitakiuka zitachukuliwa hatua kama hizi ili kukuza mpira wa nchini kwa haki,usawa na nidhamu.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.