Saturday, May 10, 2025
Home Makala Namungo Yatolewa Mapinduzi Cup

Namungo Yatolewa Mapinduzi Cup

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Namungo Fc imetolewa katika michuano ya kombe la Mapinduzi inayoendelea Visiwani Zanzibar baada ya kukubali kipigo cha mabao 5-4 kutoka kwa Mlandege katika changamoto ya mikwaju ya penati baada ya awali kutoka 1-1 katika dakika tisini za mchezo.

Iliwachukua Namungo Fc dakika saba pekee kuandika bao la kwanza lililofungwa na Ibrahim Mkoko kwa kichwa baada ya mabeki wa Mlandege Fc kuzembea kuokoa krosi iliyopigwa kutoka upande wa kushoto mwa uwanja.

Dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza Mlandege walisawazisha bao hilo kupitia kwa Bashima Saite baada ya kipa wa Namungo kuutema mpira uliopigwa langoni kwake na mfungaji kuuwahi mpira huo na kufunga kirahisi ambapo licha ya mashambulizi ya hapa na pale mpaka dakika tisini zinakamilika matokeo yalibaki hivyo hivyo.

banner

Changamoto ya mikwaju ya penati Mlandege Fc walifanikiwa kufunga zote tano huku Namungo Fc wakikosa penati moja na kuwafanya Mlandege Fc kuungana na Singida Big Stars kucheza mchezo wa fainali wikiendi hii siku ya Ijumaa Januari 13.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.