Thursday, May 8, 2025
Home Makala Tabora United Yavuna Alama 3 Namungo

Tabora United Yavuna Alama 3 Namungo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Tabora United imeibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Namungo mchezo wa ligi kuu ya NBC uliochezwa leo Agosti 25,2024 katika uwanja wa Majaliwa ulioko wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.

Namungo ilitangulia kwa bao la kwanza lililofungwa na  Mcongomani Djuma SShabani kwa penati kabla ya Heritier Makambo kuchomoa pia kwa penati na dakika za mwishoni mwa mchezo alitoa pasi ya goli kwa Salum Chuku aliyefanikiwa kufunga bao la ushindi.

Huo ni mchezo wa pili kwa Tabora United msimu huu ambapo mchezo wa kwanza walifungwa 3-0 na Simba ilhali Namungo ni mchezo wa kwanza.

banner

Tabora United baada ya kumaliza michezo ya ugenini sasa itacheza mechi zake tatu mfululizo katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi dhidi ya Kagera Sugar,Prisons na Fountain Gate.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.