Saturday, May 10, 2025
Home Makala Metacha,Beki Kisiki Watambulishwa Yanga sc

Metacha,Beki Kisiki Watambulishwa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imewatambulisha wachezaji Metacha Mnata na Seydou Doumbia kama wachezaji wapya wa klabu hiyo baada ya kuwasajili dakika za lala salama za dirisha la usajili nchini siku ya Januari 15 usiku saa sita kamili.

Yanga sc imelazimika kumsajili Metacha Mnata iliyomtema miaka miwili iliyopita baada ya kuwa na matatizo ya utovu wa nidhamu ili kuziba nafasi ya Aboutwalib Mshery ambaye amepata majeraha ya goti na anatarajiwa kuwa nje kwa muda mrefu akijiuguza majeraha hayo.

Pia usajili wa Doumbia 27′ umefanyika kwa lengo hasa la michuano ya kimataifa kutokana na beki huyo kuwa na uzoefu mkubwa katika michuano hiyo akiwa kama nahodha wa kikosi cha timu ya taifa ya wachezaji wa ndani wa Mali inayoshiriki katika michuano ya Chan nchini Algeria.

banner

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.