Thursday, May 8, 2025
Home Makala Jacob Mulee Kocha Mpya Kenya

Jacob Mulee Kocha Mpya Kenya

by Sports Leo
0 comments

Jacob Mulee ametangazwa jana Octoba 21 na Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Kenya (FKF),Nick Mwendwa kama kocha mkuu wa timu ya taifa ya Kenya Hrambee Stars.

Mulee mwenye umri wa miaka 52 amesaini kandarasi ya miaka mitatu akipokea mikoba ya Francis Kimanzi aliyeachana na miamba hao wa soka siku mbili zilizopita akiwa pamoja na benchi la ufundi.

Benchi la ufundi lililoondoka na Francis ndilo lililoiwezesha Kenya kufuzu kucheza AFCON 2019 kwa mara ya kwanza baada ya ya miaka 15.

banner

Mwendwa ana matumaini makubwa kwa Jacob kwani ni kocha anayeujua mpira wa Kenya na amekuwa hapo akiucheza,ameshinda ligi ameshinda mataji mbalimbali ikiwemo Cecafa na amekuwepo pia kwenye michuano ya AFCON hivyo anaamini watapiga hatua kubwa msimu huu wa 2020/2021 katika ligi kuu Kenya.

 

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.