Friday, May 9, 2025
Home Makala Namungo Waikaba Azam Fc Chamazi

Namungo Waikaba Azam Fc Chamazi

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imeshindwa kuchukua alama tatu muhimu katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Klabu ya Namungo Fc uliofanyika katika uwanja wa Azam Complex Chamazi baada ya kubanwa na kutoa sare ya 1-1.

Azam Fc ilishindwa kufurukuta baada ya kuruhusu bao la mapema la Hamis Halifa Nyenye dakika ya 12 kwa shuti kali lililomshinda kipa Mohamed Mustapha.

Bao halikudumu sana kwa jitihada binafsi za Feisal Salum zilisaidia kumpa pasi nzuri Gibril Sillah na kufunga bao zuri dakika ya 44 ya kipindi cha kwanza.

banner

Baada ya kutoka mapumziko mechi iliendelea kuwa nzuri na ya kuvutia huku Azam Fc wakikosa penati baada ya kipa Jonathan Nahimana kuokoa penati ya Feisal Salum.

Mpaka dakika 90 zinakamilika timu hizo ziligawana alama na Azam Fc kufikisha alama 45 katika michezo 22 nafasi ya 3 ya msimamo huku Namungo Fc wakifikisha alama 23 katika michezo 22 ya ligi kuu katika nafasi ya 12 ya msimamo.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.