Home Soka Shikhalo Atua Kmc

Shikhalo Atua Kmc

by Sports Leo
0 comments

Aliyekua kipa wa klabu ya Yanga sc Farouk Shikhalo amejiunga na klabu ya klabu ya Kmc kwa mkataba wa mwaka mmoja akiwa kama mchezaji huru baaada ya kutoongeza mkataba na klabu ya Yanga sc aliyoitumikia kwa miaka miwili.

Kipa huyo raia wa Kenya alitua nchini miaka miwili iliyopita akitokea Bandari Fc ya kenya ambapo alifanikiwa kuwa kipa bora wa msimu huo na akajiunga na Yanga sc ambapo hakuwa na namba ya uhakika bali walipokezana na Metacha Mnata ambao mwishoni walitemwa wote kwa mapendekezo ya kocha Nasredine Nabi.

Shikhalo aliyekua kipenzi cha mashabiki wa klabu ya Yanga sc atakua na jukumu la kutafuta nafasi mbele ya Juma Kaseja aliyedumu Kmc huku akitumika kama kipa chaguo la kwanza kwa misimu kadhaa sasa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.