Home Soka ‘Nkana Fc Wakipange-Namungo

‘Nkana Fc Wakipange-Namungo

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha Namungo kinaendelea na mazoezi makali kujiandaa na mchezo wao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Nkana kutokea Zambia, huku wakitamba kuwa Wazambia hao lazima wadondoshe pointi tatu kwa Mkapa.

Ofisa Habari wa Namungo, Kindamba Namlia amesema: “Kikosi chetu kinaendelea vizuri na mazoezi ya kujiandaa na mchezo wetu wa Ijumaa dhidi ya wageni wetu Nkana kutokea Zambia.

“Mpaka sasa tumekamilisha asilimia kubwa ya maandalizi ya mchezo huo na tunasubiri muda wa mchezo ufike, kikosi chetu kiko kamili kwani idadi kubwa ya majeruhi tayari wamepona na wanaendelea na mazoezi japo tutaendelea kukosa huduma ya mshambuliaji wetu Bigirimana Blaise ambaye amekuwa na majeraha ya muda mrefu.”
.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited