Wednesday, May 7, 2025
Home Makala Ngorongoro Heroes Yatwaa Ubingwa Cecafa

Ngorongoro Heroes Yatwaa Ubingwa Cecafa

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20 imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe la vijana la ukanda wa soka wa Afrika mashariki na kati (Cecafa) baada ya kuifunga Kenya kwa mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Pamoja na kupoteza mchezo huo Kenya imeungana na Tanzania kufuzu michuano ya Afcon 2025 itakayofanyika mwakani.

Ngorongoro Heroes walianza kufungwa dakika ya 47 lakini walisawazisha dakika ya 64 ya mchezo kwa bao la Valentino Mashaka aliyepokea pasi nzuri ya Shekhan Ibrahim huku Shekhan tena akifunga bao la ushindi dakika ya 82 kwa shuti kali baada ya beki wa Kenya kuokoa vibaya na mpira kumkuta mfungaji.

banner

Katika Mchezo huo vijana hao wa chini ya umri wa miaka 20 walizawadiwa fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni ishirini kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk Samia Suluhu Hassan ikiwa ni pongezi kwa ushindi huo.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.