Thursday, May 8, 2025
Home Soka Gadiel Arejea Taifa Stars

Gadiel Arejea Taifa Stars

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Cape Town Spurs ya nchini Afrika ya kusini Gadiel Michael Mbaga baada ya kukiwasha katika Klabu yake hiyo hatimaye amejumuishwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kinachokwenda kushiriki michuano ya kirafiki nchini Saudi Arabia.

Gadiel Michael ilikua ni kama karia yake ya mpira imekwisha baada ya kuzitumikia Azam,Yanga na Simba lakini ni dhahiri kwamba benchi la unyamani ndilo lililokua linataka kumaliza maisha yake ya mpira.

banner

Hata hivyo punde tu baada ya kujiunga na Singida Big Stars mwalimu Ernst Middendorp alimhamishie eneo la kiungo na kisha kumpa nafasi ya kutosha na baada ya kocha huyo kuachana na klabu hiyo na kuajiriwa na Cape Town City Spurs mara moja alimsajili mchezaji huyo na kumpa nafasi mara kwa mara ya kucheza.

Gadiel mpaka sasa ameitumikia klabu hiyo michezo takribani kumi tangu ajiunge kwa mkopo mwezi Januari mwaka huu na kufanikiwa kufunga bao moja na kutoa assisti mbili za mabao akicheza zaidi upande wa kushoto kama beki ama winga.

Beki huyo amerejea rasmi katika kikosi hicho cha Taifa Stars ambacho kesho atakwea pipa kwenda nchini Saudi Arabia kucheza michezo miwili ya kirafiki na timu ya Taifa ya Sudan.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.