Wednesday, May 14, 2025
Home Makala Simba sc Yatua Bukoba,Kuwavaa Kagera Sugar

Simba sc Yatua Bukoba,Kuwavaa Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha mabingwa mara nne wa ligi kuu nchini Simba sc kimetua mkoani Kagera kuwavaa Kagera Sugar katika mchezo wa ligi kuu nchini hapo kesho katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba huku ikipokelewa kwa shangwe na mashabiki mkoani humo.

Kikosi hicho kimetua mkoani humo kikiwa kamili na mastaa wake wote wa kikosi cha kwanza huku mtendaji mkuu wa klabu hiyo Barbara Gonzalez akiongoza msafara huo kuhakikisha wanavuna alama tatu ili kupunguza pengo la alama dhidi ya Yanga sc wanaongoza ligi kuu nchini wakiwa na alama 35.

Mashabiki mbalimbali walijitokeza uwanja wa ndege kuwapokea mastaa hao huku Ahmed Ally ambaye ni meneja wa habari akishangiliwa na mashabiki sambamba na mastaa Aishi Manula na Cletous Chama hali iliyoamsha shangwe kwa mashabiki hao baada ya kuwalaki mastaa wa kikosi hicho.

banner

Mchezo huo ulitakiwa kufanyika mwezi uliopita lakini changamoto ya kuugua ugonjwa wa mafua kwa baadhi ya wachezaji wa timu zote mbili zilisababisha mchezo huo kusogezwa mbele hadi kesho.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.