Wednesday, May 7, 2025
Home Makala Simba sc Yapaa Uturuki

Simba sc Yapaa Uturuki

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha Simba sc kimeondoka nchini jioni ya tarehe 11/7/2023 kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu na michuano ya kimataifa ambayo klabu hiyo itashiriki kuanzia msimu ujao.

Kambi hiyo muhimu kwa maandalizi ya utimamu wa mwili na kutengeneza muunganiko wa kikosi hicho ambacho mpaka sasa kimesajili mastaa takribani wanne  huku pia ikiwa na benchi jipya la ufundi chini ya mkufunzi Roberto Oliveira.

Mastaa kama Andre Onana,Aubin Kramo,Che Fondoh Malone,David Kameta watapata nafasi ya kufundishwa mbinu mpya za mwalimu Robertinho huku pia wakiangaliwa jinsi ya kutengeneza muunganiko mzuri na mastaa kama Cletous Chama na Saido Ntibanzokiza ambao kwa muda mfupi wamejenga ufalme klabuni hapo.

banner

Katika msafara huo mbali na wachezaji pia baadhi ya watalaamu wapya wa benchi la ufundi la klabu hiyo waliotambulishwa siku chache zilizopita pia wameambatana na klabu hiyo tayari kuanza kuingiza utaalamu wao kikosini humo.

Simba sc mapema mwanzoni mwa mwezi Augusti italazimika kucheza michuano ya ngao ya hisani dhidi ya Singida Fountain Gate ambapo ikishinda itakutana na mshindi kati ya Yanga sc na Azam Fc.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.