Wednesday, May 7, 2025
Home Makala Ninja Kutua Geita Gold Sc

Ninja Kutua Geita Gold Sc

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Yanga sc Abdalah Shaibu ‘Ninja’ ameuomba uongozi wa klabu ya Yanga sc kumruhusu kwenda kwa mkopo katika klabu ya Geita Gold Sc ambayo imeonyesha nia ya kumsajili kwa mkopo wa msimu mzima.

Ninja ambaye amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Yanga sc baada ya kocha Nabi kumhitaji kikosini licha ya uongozi wa klabu hiyo kuonyesha nia ya kutomuongezea mkataba ambao ulikua umeisha na tayari alikua amesharejea nyumbani kwao Zanzibar kujipanga kutafuta timu nyingine.

Geita Gold Sc ambayo itashiriki michuano ya kimataifa ya Kombe la shirikisho ipo katika harakati za kujenga kikosi chake ili kupata uhakika wa kufanya vizuri zaidi katika michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa ngazi za vilabu barani Afrika.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.