Thursday, May 8, 2025
Home Makala Mshery Kufanyiwa Upasuaji

Mshery Kufanyiwa Upasuaji

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeamua kumpeleka nchini Morroco golikipa wake namba mbili AbouTwalib Mshery ambaye anasumbuliwa na goti ili apone haraka ambapo atafanyiwa upasuaji na wataalamu wabobezi wa masuala ya viungo.

Maamuzi hayo yamefikiwa kutokana na umuhimu wa kipa huyo wakati klabu hiyo ikielekea katika michuano ya kimataifa ambapo mpaka sasa inao makipa wengine watatu wakiongzowa na Djigui Diarra,Metacha Mnata ambaye yupo kwa mkopo wa miezi sita na Erick Johora.

Wataalamu hao ambao watamfanyia matibabu kipa huyo ni wale ambao walimtibu Kibwana Shomari na Yacouba Songne ambao nao walikua wakisumbuliwa na magoti.

banner

Mshery tangu asajiliwe Yanga sc amefanikiwa kuwa mbadala wa kudumu wa Djigui Diarra ambaye hata anapokosekana kinda huyo hufanya kazi nzuri inayowavutia mashabiki wa soka nchini.

You may also like

Leave a Comment

Soledad is the Best Newspaper and Magazine WordPress Theme with tons of options and demos ready to import. This theme is perfect for blogs and excellent for online stores, news, magazine or review sites.

Buy Soledad now!

Edtior's Picks

Latest Articles

u00a92022u00a0Soledad.u00a0All Right Reserved. Designed and Developed byu00a0Penci Design.