Connect with us

Makala

Beki Katili Atambulishwa Simba sc

Klabu ya Simba sc imekamilisha usajili wa beki Mohamed Ouatarra kutoka klabu ya Al Hilal ya nchini Sudan kwa mkataba wa miaka miwili akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Serge Pascal Wawa ambaye amepewa mkono wa kwaheri na sasa amejiunga na klabu ya Singida Big Stars.

Awali Simba sc ilihusishwa na beki Hervé Ngomo wa CotonSports ya nchini Cameroon lakini ujio wa kocha mpya Zoran Maki ulibadili usajili huo ambapo alimtaka Ouatarra ambaye anamfahamu vizuri na hivyo klabu hiyo kuachana na Ngomo.

Kwa sasa klabu ya Simba sc ipo katika kambi ya maandalizi ya msimu mpya nchini Misri ambapo pia mchezaji huyo nae moja kwa moja ameungana na kikosi kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu nchini huku pia wakitarajiwa kucheza mchezo wa utambulisho wa wachezaji siku ya August 8 na siku tano baadae watavaana na Yanga sc katika kufungua dimba la msimu mpya nchini katika mchezo wa ngao ya jamii.

Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

More in Makala