Home Makala Bongo Zozo Atua Lipuli Fc

Bongo Zozo Atua Lipuli Fc

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa Timu ya Lipuli FC ya mkoani Iringa imemtangaza shabiki na mhamasishaji wa Timu ya taifa ya Tanzania Nick Reynolds maarufu kama Bongo zozo kuwa Balozi wake kwa lengo la kuitangaza timu ya Lipuli FC pamoja na kusaidia wachezaji wake kucheza Kimataifa.

“Nimependa na nitaenda kufanya kazi, nitasafisha njia ili wachezaji wawe na uwezo wa kuonesha utaalamu wao, unaweza kuwa mchezaji mzuri sana lakini Waingereza hawakujui lakini mimi nitasafisha njia”, amesema Bongo Zozo.

Bongo zozo amesaini mkataba huo mbele ya waandishi wa habari makao makuu ya klabu hiyo mkoani Iringa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited