Home Makala Hamza kamili Gado Kuwavaa Rs Berkane

Hamza kamili Gado Kuwavaa Rs Berkane

by Sports Leo
0 comments

Beki wa kati wa Simba Sc  Abdulrazack Hamza (22) amefanya mazoezi na wachezaji wenzake kwaajili ya mechi ya pili ya  Fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya RS Berkane utakaofanyika siku ya Jumapili Mei 25 2025 katika uwanja wa Amaani Visiwani Zanzibar.

Hamza Baada ya kushindwa kumaliza mechi ya Fainali ya kwanza pale Morocco, sasa yupo tayari kwaajili ya mechi ya pili ambapo amefanikiwa kushiriki mazoezi na wenzake akiwa fiti kabisa.

Sasa kocha Fadlu Davis atakua na wigo mpana wa kuchagua kati ya Hamza na Che Malone Fondoh pamoja na Chamou Karabou kuona nani anaweza kuanza katika mabeki wawili wa kati.

banner

Simba sc itakua na wakati mgumu ikitafuta kupindua meza baada ya kuruhusu mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika nchini Morocco.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited